Print this page
WANAJUMUIYA WA CHUO KIKUU MZUMBE AHIMIZWA KUENZI MICHEZO
09 June 2022 Published in News Written by 

WANAJUMUIYA WA CHUO KIKUU MZUMBE AHIMIZWA KUENZI MICHEZO

Rate this item
(0 votes)
Be the first to comment!

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Lughano Kusiluka amewataka Wanafunzi na Wanajumuiya wote wa chuo Kikuu Mzumbe kuienzi na kushiriki katika michezo mbalimbali inayoandaliwa chuoni hapo kwani michezo ni muhimu sana kwa afya zao kwa kuwa huwaepusha na magonjwa.

Prof. Kusiluka amesema hayo katika sherehe za ufunguzi wa mashindano ya vitivo (Inter-faculty Games 2022) yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya michezo vilivyopo kampasi kuu Morogoro ambapo pia ameahidi kuboresha miundombinu ya michezo ikiwa ni pamoja na kununua vifaa mbalimbali vya michezo.

 “Menejimenti ya Chuo ina maono ya muda mrefu kuhusu michezo  kwa kuwa ni fursa kubwa ya kujitangaza na pia ni muhimu  kwa ajili ya afya zetu, pia tutambue kuwa michezo ni ajira na utajiri, kwahiyo tuendelee kuienzi michezo ”.Alisisitiza. 

 Katika hatua nyingine Makamu Mkuu wa Chuo amewapongeza Wanamichezo wote walioshiriki katika michezo ya TUSA mkoani Dodoma na kufanikiwa  kutwaa medali nyingi na kusema kuwa ana imani mwaka huu Wawakilishi hao wataleta medali nyingi zaidi.

Ufunguzi wa mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka ulihusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete, (Volleyball) na mpira wa kikapu na kuhudhuriwa na Wadau wa michezo wakiwemo Wafanyakazi wa Chuo Kikuu Mzumbe, Wanafunzi kutoka vitivo na skuli mbalimbali, Serikali ya wanafunzi na Wanajumuiya wengineo wa chuo kikuu Mzumbe.

****************************************************************************************************************************************************************************************

 

Read 1473 times
Last modified on Thursday, 29 September 2022 08:19