mzumbe
Baadhi ya picha za Kikao Kazi cha kuboresha daftari la vihatarishi, Kikao kazi hiyo kilihusisha wawakilishi kutoka katika Vitivo, Ndaki, Kurugenzi na Vitengo kutoka Chuo Kikuu Mzumbe na kufanyika katika Hotel ya Oasis Morogoro 7.12.2023
Mzumbe University invites applications from suitably qualified and competent Tanzanians to feel the following fifteen vacancies in academic positions at University.
CALL FOR APPLICATION INTO POSTGRADUATE PROGRAMMES OF THE MZUMBE UNIVERSITY FOR THE ACADEMIC YEAR 2023/2024 FOR THE OCTOBER, 2023 INTAKE
The Directorate of Research, Publications and Postgraduate Studies (DRPS), Mzumbe University invites applications for admission to the postgraduate programmes (Masters and Doctoral degree Programmes) for the 2023/2024 academic year from qualified candidates.
A: MASTER’S DEGREE PROGRAMMES
Master’s degree programmes are offered at three campuses: the Main Campus (Mzumbe, Morogoro), Dar es Salaam Campus (at Upanga, Dar es Salaam City) and Mbeya Campus (at Forest, Mbeya City). All programmes offered at Mzumbe Main Campus are fulltime, day sessions mode and residential but due to limited accommodation, some successful applicants may be required to seek for alternative accommodation off campus. The Dar es Salaam Campus offers day, evening, and executive mode classes, while the executive mode is for MBA and MPA programmes only. Mbeya Campus offers evening mode classes only. Both Dar Es Salaam and Mbeya Campuses do not have accommodation arrangements for the students, they are non-residential. THE DEADLINE FOR SUBMITTING APPLICATION FOR MASTER’S DEGREE PRGRAMMES IS 29TH OCTOBER, 2023.
For more details, Click here
For Non- Degree Programmes offered at Main Campus Morogoro and Mbeya Campus, Click here
VIJANA KUNUFAIKA NA MITAJI YA UFADHILI WA UMATI (“CROWDFUNDING”)
Serikali imeahidi kuendelea kuandaa mazingira wezeshi, pamoja na kuharakisha uundwaji wa Sera na miongozo itakayosaidia wajasiriamali vijana, kuanza kunufaika na mpango wa upatikani mikopo kwa njia ya mtandao (Crowdfunding), pamoja na kuhakikisha fedha zitakazokusanywa zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.
Hayo yameelezwa Dkt. Mursali Milanzi, mgeni rasmi, akimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, wakati wa ufunguzi wa Warsa ya siku moja iliyoandaliwa na Chuo Kikuu Mzumbe, wakati wa kuwasilisha matokeo ya utafiti. Warsha hiyo ilifanyika katika ukumbi Royal Village, Dodoma na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sekta ya fedha ikiwemo Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana.
Milanzi, amepongeza Chuo Kikuu Mzumbe kwa kubuni utafiti ambao utasaidia vijana kupata mitaji na kutatua changamoto kubwa ya mitaji kwa vijana, na kwamba utafiti huo utasaidia sana Serikali katika kuhuisha na kuandaa Sera na miongozi itakayotoa dira ya namna ya upatikanaji wa mitaji yenye riba na masharti nafuu, kwa makundi mbalimbali yaliyopo katika jamii kwa njia ya mtandao.
Akimkaribisha mgeni Rasmi, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof. William Mwegoha, amesema lengo la mradi huo ni kuelewa namna bora ya kukuza na kuendeleza biashara zinazoanzishwa na kuongozwa na vijana, kupitia upatikanaji wa mitaji ya ufadhili wa umati (Global Funding) kwa njia ya mtandao wa mawasiliano (internet), kuelewa tabia na vipaumbele vya wafadhili wa umati katika muktadha wa umbali mkubwa kijiongorafia, na tofauti za kitamaduni kati ya wahitaji wa mitaji na wafadhili wa mitaji, pamoja na kuelewa mikakati gani ni mizuri katika kuhakikisha vijana wa Kitanzania wananufaika na upatikanaji wa mitaji kupitia ufadhili wa umati kwa njia ya mtandao (internet), ambapo baadhi ya nchi za Afrika tayari zimeanza kunufaika na mpango huo.
Akiwasilisha matokeo ya utafiti huo, Mratibu wa Mradi huo Dkt. Nsubili Isaga, amesema mikoa iliyohusika katika utafiti huo ni Dar es salaam, Morogoro, Mbeya, Arusha na Mwanza, na matokeo ya awali yanaonesha idadi kubwa ya vijana hawatambui fursa hizo, wakati Utamaduni ukiathiri kwa sehemu kubwa uwepo wa utaratibu mzuri wa kuchangia maendeleo ya vijana kwa njia ya Umati.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Mwakilishi kutoka Idara ya Maendeleo ya Sekta ya Fedha, Bi.Dionisia Mjema na Mwakilishi kutoka Soko la Mitaji, Bw. Charles Shirima, wamesema utafiti huo umekuja muda muafaka katika kuhakikisha soko la mitaji linakua na vijana wanatambua fursa mbalimbali zilizopo. Tayari hatua mbalimbali zimeshaanza kuchukuliwa na Serikali kwa kutunga Sera, Kanuni na Taratibu zinakazosaidia vijana wengi kunufaika na mpango huo pamoja na kujiepusha na makosa ya kimtandao ukiwemo wizi na utapeli.
Warsha hiyo ilihudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo kutoka taasisi mbalimbali za Serikali, Mashirika Binafsi na Taasisi ya Fedha yakiwemo Mashirika yanayojihusisha moja kwa moja na maendeleo ya Vijana.
Mradi unatekelezwa na Chuo Kikuu Mzumbe, kupitia Skuli ya Biashara, Idara ya Uhasibu na Fedha kwa ufadhili wa Serikali ya Denmark, kupitia "Danida Fellowship Centre”, na unategemewa kumalizika Januari 2024 Mradi huu.
******************************************
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Lughano Kusiluka amewataka Wanafunzi na Wanajumuiya wote wa chuo Kikuu Mzumbe kuienzi na kushiriki katika michezo mbalimbali inayoandaliwa chuoni hapo kwani michezo ni muhimu sana kwa afya zao kwa kuwa huwaepusha na magonjwa.
Prof. Kusiluka amesema hayo katika sherehe za ufunguzi wa mashindano ya vitivo (Inter-faculty Games 2022) yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya michezo vilivyopo kampasi kuu Morogoro ambapo pia ameahidi kuboresha miundombinu ya michezo ikiwa ni pamoja na kununua vifaa mbalimbali vya michezo.
“Menejimenti ya Chuo ina maono ya muda mrefu kuhusu michezo kwa kuwa ni fursa kubwa ya kujitangaza na pia ni muhimu kwa ajili ya afya zetu, pia tutambue kuwa michezo ni ajira na utajiri, kwahiyo tuendelee kuienzi michezo ”.Alisisitiza.
Katika hatua nyingine Makamu Mkuu wa Chuo amewapongeza Wanamichezo wote walioshiriki katika michezo ya TUSA mkoani Dodoma na kufanikiwa kutwaa medali nyingi na kusema kuwa ana imani mwaka huu Wawakilishi hao wataleta medali nyingi zaidi.
Ufunguzi wa mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka ulihusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete, (Volleyball) na mpira wa kikapu na kuhudhuriwa na Wadau wa michezo wakiwemo Wafanyakazi wa Chuo Kikuu Mzumbe, Wanafunzi kutoka vitivo na skuli mbalimbali, Serikali ya wanafunzi na Wanajumuiya wengineo wa chuo kikuu Mzumbe.
***************************************************************************************************************************************************************************************
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Lughano Kusiluka amewataka Wanafunzi na Wanajumuiya wote wa chuo Kikuu Mzumbe kuienzi na kushiriki katika michezo mbalimbali inayoandaliwa chuoni hapo kwani michezo ni muhimu sana kwa afya zao kwa kuwa huwaepusha na magonjwa.
Prof. Kusiluka amesema hayo katika sherehe za ufunguzi wa mashindano ya vitivo (Inter-faculty Games 2022) yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya michezo vilivyopo kampasi kuu Morogoro ambapo pia ameahidi kuboresha miundombinu ya michezo ikiwa ni pamoja na kununua vifaa mbalimbali vya michezo.
“Menejimenti ya Chuo ina maono ya muda mrefu kuhusu michezo kwa kuwa ni fursa kubwa ya kujitangaza na pia ni muhimu kwa ajili ya afya zetu, pia tutambue kuwa michezo ni ajira na utajiri, kwahiyo tuendelee kuienzi michezo ”.Alisisitiza.
Katika hatua nyingine Makamu Mkuu wa Chuo amewapongeza Wanamichezo wote walioshiriki katika michezo ya TUSA mkoani Dodoma na kufanikiwa kutwaa medali nyingi na kusema kuwa ana imani mwaka huu Wawakilishi hao wataleta medali nyingi zaidi.
Ufunguzi wa mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka ulihusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete, (Volleyball) na mpira wa kikapu na kuhudhuriwa na Wadau wa michezo wakiwemo Wafanyakazi wa Chuo Kikuu Mzumbe, Wanafunzi kutoka vitivo na skuli mbalimbali, Serikali ya wanafunzi na Wanajumuiya wengineo wa chuo kikuu Mzumbe.
****************************************************************************************************************************************************************************************
Mzumbe University will hold its 1st Mini- Graduation Ceremony at Main Campus, Thursday, 24th June 2021, New Assembly Hall - NAH (Samora ) starting from 10.00am.
The ceremony will be presided by the Chancellor of Mzumbe University, former President of Zanzibar and Chairman of Revolutionary Council, His Excellence Dkt Ali Mohamed Shein. Candidates who successfully completed their studies from all our three campuses, and qualified for the award of Certificates, Diplomas and Degrees of Mzumbe University for the 2020/2021 Academic Year will be conferred their respective awards.
Graduation rehearsals will be held as follows:
- Main Campus: Wednesday, 23rd June 2021 at NAH Assembly Hall, starting from 2.00 pm.
For more details,Click here
Mzumbe University invites applications from suitably qualified Public Servants who wish to be transferred to Mzumbe University as Academic Staff at the level of Assistant Lecturer in the areas of specialization indicated below:-
Mr Stephen Nalailas's profile
Dr Ubena John's Profile
Address
Mzumbe University,
Faculty of Law,
P.O. Box 9,
Mzumbe - Morogoro
Tanzania
Phone: +255 -23-260- 4380/1/3/4
Mobile: +255 714 404496 Fax: +255-23-260-4382
E-mail: juThis email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. or This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
Consultation: Monday 11:00AM - 13:00PM
Office: Faculty of Law Building Office No. 21, Mzumbe University (Main Campus) Mzumbe Morogoro